Kutoa ni moyo na sio utajiri.....Wanafunzi chuo kikuu Iringa kumchangia mwenzao kutokana na juhudi alizo onyesha kwao

 

Wengi waonyesha  kuguswa juu ya uelekeo wa mwanafunzi Chuo Kikuu Iringa.

Wanafunzi wa kitivo cha sanaa ya sayansi na mahusiano ya jamii hususani wale wa shahada ya Uandishi wa Habari na Utangazaji mwaka wa tatu katika  chuo kikuu cha Iringa waonyesha kuguswa juu ya jitihada zilizofanywa na mmoja wa wanafunzi chuoni hapo juu ya uelekeo wake kielimu alionao.
Mwanafunzi huyo ajulikanae kwa jina la Joel John Haule ambaye ni mlemavu wa miguu hutegemea zaidi baiskeli ndogo kutembelea kwa msaada wa kusukumwa  anasoma stashahada (Diploma) ya maendeleo ya jamii chuoni hapo kwa mwaka wa kwanza sasa amekua akifanya vizuri sana darasani hivyo kupelekea wanafunzi wenzake kuweza kuguswa na kujitolea kumchangia kiasi cha pesa ili kiweze kumsaidia katika matumizi madogodogo chuoni hapo kutokana na kukosa msaada zaidi wa kifedha na mahitaji mengine juu ya elimu yake.
Wanafunzi hao waliweza kuchanga kiasi cha Tsh.69,000/= kwa ghafla muda waliokua darasani kuweza kumsaidia mwenzao huyo wazo lililotolewa na mmoja wa wanafunzi wa uandishi wa habari Tumaini Msowoya wakiwa katika mjadala uliotokana na somo lililokuwa likifundishwa na mwalimu Mr. Nduye M. ambaye ndiye mwalimu wa somo la kanuni za ufundishaji (Principle of Teaching).
Wazo hilo lilitiliwa mkazo na kufafanuliwa zaidi na mwalimu huyo mpaka kupelekea wengi wa wanafunzi hao kujikuta wakiguswa kitendo kilicho pelekea wao kuamua kumchangia mwanafunzi huyo.
Hata hivyo Joel aliweza kuwashukuru wanafunzi hao kwa ukarimu walionao na kuweza kuonyesha hisia zao juu ya watu wenye ulemavu kuwaona kuwa nao kumbe wanaweza katika elimu hususani elimu ya juu, pia aliweza kutoa ushauri kwa watu wenye ulemavu kama yeye kuweza kujitangaza (expose) kwa jamii juu ya ulemavu wao ili waweze pata misaada na mawazo mbali mbali ili waweze kujichanganya na watu wengine ambao sio walemavu ili waweze kubadilika na si kujitenga na kukaa kwa mawazo kutokana na hali waliyonayo. 
Joel mpaka sasa anakabiliwa na tatizo la kifedha zaidi kutokana na maumbile aliyonayo ya ulemavu wa miguu hivyo kumpelekea kuto jiingiza katika shughuri za kuingiza kipato ili kuweze kumkidhi katika mahitaji yake ya kimaisha .
Pia anahitaji msaada zaidi juu ya maisha aliyonayo chuoni hapo katika mazingira ya ada ya chuo, chakula, mavazi pamoja na fedha za steshonari ili kuweza kufanikisha malengo yake kwani anataraji kusoma na kuweza kufika katika ngazi ya juu kielimu. Hivyo kwa wale wote waliotayari kujitolea waweza tuma msaada wako kupitia namba yake ya simu ya mkononi ambayo ni 0769694831 (kwa njia ya M-Pesa). 



0 comments:

Post a Comment